• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua pepe |
BUTIAMA DISTRICT COUNCIL
BUTIAMA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Mungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA BUTIAMA

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
  • Utawala
  • Investment Opportunities
  • Huduma
  • Councillors
  • Miradi
  • Media Centre

Historia

Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ilianzishwa mwezi Agosti 2013, kabla ya hapo ilikuwa ni sehemu ya Halmashauri ya Wilaya ya Musoma vijijini. Halmashauri hii ndipo alipozaliwa baba waTaifa la Tanzania hayati Mwl.Julius Kambarage Nyerere.

Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ina jumla ya eneo la kilometa za mraba 2,257.127. Kati ya eneo hilo kilometa za mraba 103 limefunikwa na ziwa Victoria.

Butiama kama yalivyo maeneo mengine ya kanda yaziwa hasa katika mkoa wa Mara ina misimu miwili tu ya mvua, kwa maana ya mvua za vuli ambazo hunyesha kati ya mwezi wa Oktoba hadi Desemba, na msimu mwingine wa mvua ni mvua za masika ambazo hunyesha kuanzia mwezi Machi hadi  mwezi Mei.

Halmashauri ya Wilayaya Butiama ina nyuzi joto za sentigredi kati ya 24 na 32.

Wakazi wa Halmashauri hii wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kilimo, ufugaji, biashara, uvuvi pamoja na uchimbaji wa madini.

Mazao ya kilimo yanayopatikana Butiama ni mahindi, viazi mviringo, viazi vitamu n.k.

MUUNDO WA UTAWALA BUTIAMA

Halmashauri ya Wilaya ya Butiama inajumla ya tarafa mbili (2), kata kumi na nane(18), vijiji hamsini na tisa(59)  na vitongoji mia tatu na sabini (370). Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ndiye kiongozi mkuu wa taasisi akisaidiwa na wataalamu mbalimbali wa Halmashauri kwa maana ya wakuu wa Idara na vitengo.

Halmashauri ya Wilaya ya Butiama ina jumla ya Idara kumi na mbili na vitengo sita. Idara hizo ni hizi zifuatazo; Idara ya Utumishi na Utawala, Idara ya Mipango, takwimu na ufuatiliaji, Idara ya Afya, Idara ya Fedha na biashara, Idara ya Elimu msingi, Idara ya Elimu sekondari, Idara ya Kilimo ushirika na umwagiliaji, Idara ya Mifugo na uvuvi, Idara ya Ardhi na mal iasili, Idara ya Maendeleo ya jamii, Idara ya ujenzi na Idara ya Maji.

Pamoja na Idara hizo Halmashauri ya Butiama ina vitengo vifuatavyo; Kitengo cha sheria, Kitengo cha ukaguzi wa ndani, Kitengo cha Teknolojia ya habari na mawasiliano, Kitengo cha ugavi,Kitengo cha uchaguzi na Kitengo cha ufugaji nyuki.

Matangazo

  • TANGAZO LA JINSI YA KUOMBA LESENI YA BIASHARA KWA KUTUMIA MFUMO WA TAUSI June 29, 2023
  • TANGAZO LA MAJINA NA MIPAKA YA VIJIJI NA VITONGOJI BUTIAMA DC September 16, 2024
  • TANGAZO LA SHERIA NDOGO VIBALI VYA UJENZI BUTIAMA DC. January 27, 2025
  • TANGAZO LA SHERIA NDOGO VIBALI VYA UJENZI BUTIAMA DC. January 27, 2025
  • Zaidi

Habari mpya

  • MAFUNZO KWA WATAALUMU WASIMAMIZI WA MIKOPO NGAZI YA KATA BUTIAMA DC.

    October 09, 2024
  • MAFUNZO KWA WATAALUMU WASIMAMIZI WA MIKOPO NGAZI YA KATA BUTIAMA DC.

    October 09, 2024
  • Mara yafikia asilimia 95.5 matumizi fedha za lishe

    August 22, 2024
  • ZOEZI LA UHAKIKI WA PIKIPIKI ZILIZOTOLEWA NA WIZARA YA KILIMO

    July 26, 2023
  • Zaidi

Video

Alichokisema Mhe.Rais ,Mama Samia suluhu Hassan alipofika Butiama kwenye ziara
video

Viunganishi vya haraka

  • MAKUMBUSHO YA BABA WA TAIFA
  • WIZARA YA TAMISEMI
  • SECRETARIET YA AJIRA (KUTAFUTA KAZI)
  • KUPATA SALARY SLIP KWA WATUMISHI WA SERIKALI

Viunganishi Muambata

  • Mkoa wa Mara
  • Utumishi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani
  • Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Butiama District Council

    Anuani ya posta: P.O.BOX 1207 BUTIAMA

    Simu: (028)2623121

    Simu: 0767300061/756357458

    Barua pepe: ded@butiamadc.go.tz

Other Contacts

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • sera
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Butiama.Haki zote zimehifadhiwa